Ugonjwa wa Corona wazua hofu Afrika, mashirika kadhaa ya ndege yasitisha safari za China

by

Mashirika mawili ya ndege barani Afrika, Kenya Airways na Rwandan Air, yamechukua uamuzi wa kufuta safari zote kuelekea na kutoka China kwa muda usiojulikana. Virusi vya Corona vimeua watu zaidi ya 200 nchini China.

Kenya Airways imesema kuwa bado iko kwenye mazungumzo na wizara ya afya na wizara ya mambo ya nje kuhusu muda ambao ndege hizo zitaacha safari ya China.